Maafisa wa polisi wasimamishwa kazi Kenya kwa kifo cha Albert Ojwang

GEORGE MARATO TV
0

 


Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS) nchini Kenya imewasimamisha kazi maafisa watano walioko katika kituo kikuu cha polisi mjini Nairobi kuhusiana na kifo cha Albert Omondi Ojwang ambaye aliaga dunia akiwa kizuizini.

Katika taarifa ya waandishi wa habari iliyotolewa Jumatatu, Juni 9, NPS ilithibitisha kusimamishwa kwa Afisa Mkuu wa Kituo cha Polisi, OCS, afisa aliyekuwa kazini usiku huo, afisa anayesimamia seli, na maafisa wote ambao walikuwa kazini usiku huo.

Inspekta Mkuu wa Polisi, Douglas Kanja, aliagiza kuchukuliwa kwa hatua hiyo kuruhusu uchunguzi ufanyike kwa ukamilifu, usio na upendeleo, na wa haraka juu ya suala hilo ambao unaongozwa na chombo huru cha kusimamia polisi nchini Kenya (IPOA).

" Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS) bado imejitolea kuhakikisha utekelezaji wa sheria, haki za binadamu, uwazi, na uwajibikaji ndani ya huduma hii," alisema taarifa ya NPS.

IPOA imeanzisha uchunguzi kuhusu kifo Ojwang ambaye alikuwa amezuiliwa "kwa uchapishaji wa taarifa za uongo.

Babake Ojwang, Meshack Opiyo aliwaambia waandishi wa habari kuwa mwanaye alikamatwa kutokana na chapisho kwenye mtandao wa X katika mji wa magharibi wa Homa Bay na kisha kusafirishwa kilomita 350 hadi mji mkuu, Nairobi.

Awali, taarifa ya polisi ilieleza kuwa, "Akiwa kizuizini, mshukiwa alipata majeraha kichwani baada ya kujigonga kwenye ukuta wa seli," Alikimbizwa hospitalini "ambapo alitangazwa kuwa amefariki dunia".

Mkurugenzi wa shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International tawi la Kenya aliiambia BBC kwamba kifo cha Bw Ojwang, aliyeelezwa kama mwalimu na mwanablogu, "kinatia shaka sana".

Amnesty ilisema katika taarifa yake kwamba kifo chake "kinaibua maswali mazito ambayo lazima yachunguzwe kwa haraka, kwa kina na kwa uhuru".

Haijabainika shtaka la "uchapishaji wa uwongo" lilirejelea nini, lakini Bw Opiyo aliambia tovuti ya mtandaoni ya Citizen Digital kwamba afisa wa polisi aliyemkamata alisema "Albert alikuwa amemtusi mtu mkuu kwenye mtadao wa X".

Akirejelea mazingira ya kukamatwa kwake, mkurugenzi wa Amnesty International Kenya, Irungu Houghton alisema ni jambo la kushangaza sana kwamba Bw Ojwang hakuwekwa katika kituo cha polisi cha eneo hilo baada ya kuzuiliwa, badala yake alichukuliwa kwa safari ndefu.

Wiki iliyopita, msanifu  Rose Njeri - ambaye aliunda jukwaa la kusaidia watu kupinga muswada wa fedha wa serikali - alishtakiwa kwa kukiuka sheria ya uhalifu wa mtandaoni.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top