Maafisa wa Jeshi la Polisi Dawati la Jinsia na Watoto Walipongeza Shirika la Hope For Girls and Women Tanzania

GEORGE MARATO TV
0



 Fresha Kinasa-Mara.

Maofisa wa  Polisi Dawati laJinsia na Watoto Walipongeza Shirika la Hope for Girls and women in Tanzania kupambana na Ukatili Mara.

Zaidi ya Maofisa wa Polisi  200  kutoka Mikoa  yote ya   Tanzania  bara na Visiwani  wanaohusika na Dawati la Jinsia na Watoto wametembelea kituo cha Nyumba Salama kiabakari' kilichopo Wilaya ya Butima Kinachotoa hifadhi kwa Wasichana waliokimbia vitendo vya Ukatili  ukiwemo ukeketaji kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mara.  

Maofisa  hao wametembelea kituoni hapo Dicemba 11, 2024 Ambapo wakiwa katika  kituo hicho  ambacho kinamilikiwa na Shirika la Hope for Girls and Women in Tanzania, (HGWT)  wamepongeza kazi   zinazofanywa na Shirika hilo  ikiwemo  kuwapa hifadhi Wasichana hao,  elimu ya ukatili, haki zao na  msaada wa kisaikolojia.

Pia,  hatua ya Shirika hilo katika  kuwaendeleza kifani na  kitaaluma, pamoja na  juhudi za utoaji wa elimu ya ukatili kwa Jamii ili kutokomeza vitendo hivyo  ambavyo ni kinyume cha sheria za nchi  na haki za binadamu.

Akizungumza na Wasichana hao Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi kutoka Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es laam  (SSP) Anitha Semwano  amewapongeza Wasichana hao kwa uamzi wa kukimbia ukeketaji kutoka katika familia zao  na kwenda kupata hifadhi katika kituo hicho. Huku pia  akiwaomba kujitambua na kutumia vyema fursa ya kuwa kituoni hapo kwa manufaa yao ya baadaye. 

"Nafurahi kuwaona Watoto mna furaha kubwa mkipata hifadhi hapa, pia napongeza huduma nzuri mnazopata hapa ikiwemo  malezi bora kutoka kwa Mkurugenzi Rhobi Samwelly. Hakika anafanya kazi kubwa licha ya kuwa na watoto wengi amewajenga kujiamini na kuishi kwa upendo."amesema.

Pia, ametoa wito kwa Jamii kushiriki kikamilifu kuwalinda Watoto wa kike dhidi ya ukeketaji na aina mbalimbali za ukatili. Huku  akihimiza mila mbalimbali zenye  madhara ziachwe kwa sababu hazina faida. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika hilo Rhobi Samwelly  amelipongeza Jeshi la Polisi kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto Mkoani humo kwani wameendelea kufanya kazi kwa karibu na kwa ushirikiano ikiwemo kutoa elimu ya ukatili wa Kijinsia katika Jamii na kuwaokoa Wasichana katika hatari ya kukeketwa. 

Aidha,  Rhobi ameongeza kuwa  kuanzia Dicemba Mosi, 2024, hadi Dicemba 10, 2024, wasichana 246, wamepokelewa na Shirika hilo katika vituo vyake vinavyotoa hifadhi  kutoka katika familia zao baada ya kukimbia ukeketaji.

Ambapo,   kituo cha Hope Mugumu Nyumba Salama wasichana 45, kituo cha Nyumba Salama kiabakari wasichana 189 na msimu huu ni wa ukeketaji ambapo Koo nyingi zinakeketa na ameiomba Watoto wa kike wasomeshwe na kuwezeshwa kusudi watimize ndoto zao.    

Rhobi Mwita ambaye ni mmoja wa Wasichana wanaopata hifadhi katika kituo hicho amewaomba Maofisa hao wa Polisi,  kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi katika kushughulikia ulinzi na usalama wa mtoto kwani dhamana hiyo wamepewa na Mwenyezi Mungu.  

Maofisa hao, wamepata fursa ya kusikiliza shuhuda mbalimbali kutoka kwa wasichana hao waliokimbia ukeketaji na kula nao chakula cha pamoja.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top