Hatimaye UVCCM yahitimisha matembezi na kilele cha mbio za mwenge Nyerere day mwanza

GEORGE MARATO TV
0

 


Na Helena Magabe.

Vijana zaidi ya 1400  wa UVCCM kutoka Mikoa mbali mbali Nchini Tanzania bara pamoja  na Visiwani walianza matembenzi  ya zaidi ya kilometa 200 Oktoba 8 2024 kutoka Butiama Mkoani Mara  kuelekea Mwanza lengo likiwa ni kuenzi kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere.

Matembenzi hayo yamezinduliwa na mgeni rasmi Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Rehema Sombi Wilaya Butiama ambapo alima sema lengo ni kuenzi kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere pamoja na kuelekea wiki ya Vijana na kilele cha mbio za mwenge na uhuru .


Alisema  mwaka 1967 katika ofisi   ya Kata ya CCM Mwitongo  Baba wa Taifa alianzia hapo matembenzi hadi Jijini Mwanza hivyo walitumia  fursa hiyo kumuenzi ikiwa ni pamoja na kuhamasisha Vijana kugombea  na kuhamasisha Vijana wenzao kushiriki uchanguzi wa Serikali za Mitaa ifikapo Novemba 27.

Aidha alisema  kilele cha matembenzi hayo ni oktoba 14 katika viwanja vya Ccm Kirumba na mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan na kuongeza kuwa iwe nvua au jua UVCCM itahakikiaha inailinda amani ya Tanzania.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top