Skip to main content

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Fahamu Jinsi Umeme wa Solar na Uoteshaji wa Mbegu Kwenye Kitalu Unavyosaidia Katika Kilimo Cha Tija

 

Na Emmanuel Chibasa

Katika jamii ya wakulima wadogo wadogo, matumizi ya kilimo cha umwagiliaji ni mbinu muhimu kwa ajili ya kukuza mazao ya mboga mboga na matunda. Hata hivyo, wakulima wengi wanakabiliwa na changamoto kutokana na mbinu wanazotumia. Kwa mfano, baadhi yao wanapanda mbegu moja kwa moja shambani, huku wengine wakipendelea kuotesha kwenye kitalu kabla ya kuhamishia miche shambani.

Kwa mujibu wa wizara ya kilimo, sekta ya kilimo kwa mwaka 2023 ilikua kwa asilimia 4.2 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 3.3 mwaka 2022 huku ikito ajira kwa wananchi kwa wastani wa asilimia 65.6 na kuchangia asilimia 65 ya malighafi za viwanda.

Licha ya uwepo wa hekta 727,280.6 za kilimo cha umwagiliaji na serikali kuweka mazingira wezeshi kwa wakulima wadogo kuendesha shughuli zao za kilimo kwa kutumia wataalam pamoja na upatikanaji wa vifaa vya nishati ya umeme jua(solar) lakini bado wakulima wadogo wanakabiliwa na changamoto katika kilimo cha tija.



Habari hii inachunguza faida na athari za mbinu hizi pamoja na ushauri kutoka kwa mtaalamu wa kilimo ili kuboresha mazao ya wakulima wdogo katika mazao mboga mboga na matunda, na pia matumizi ya solar.

Mwandishi wa George Marato Tv amezungumza na baadhi ya wakulima wanaoendesha shughuli za kilimo katika kijiji cha nywatwali wilayani bunda mkoani Mara na kukukutana na Beatrice Nyamhokya ambaye ni mkulima wa mboga mboga anaendesha kilimo cha umwagiliaji na anatumia mbinu ya kuotesha mbegu kwenye kitalu kabla ya kuhamishia miche shambani.

Ingawa Beatrice anaendesha shughuli za kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia pump za mafuta kumwagilia mazao yake, lakini  anasema pump hiyo inatumiwa na wakulima wengine katika eneo hilo kaatika kumwagilia mazao yao.

Amesema kuotesha mbegu kwenye kitalu kunamwezesha kupata miche yenye afya na rutuba, ambayo ina uwezo mkubwa wa kustahimili magonjwa na wadudu pindi anapoihamishia shambani kwa ajili ya ukuaji. Anaeleza faida za mbinu hii ni pamoja na ongezeko la uzalishaji, mazao bora, na muda mdogo wa kupanda tena baada ya mavuno lakini changmoto kubwa anayokumbana nayo ni gharama za umwagiliaji kutokana na kutumia pump ya mafuta na pesa nyingi inatumika kununua mafuta.

"Kwa kutumia kitalu, naweza kudhibiti mazingira ya ukuaji wa miche yangu na kuhakikisha kuwa inakuwa na afya njema kabla ya kuhamishia shambani. Hii inasaidia kupata mavuno yenye ubora wa hali ya juu lakini changamoto ni umwagiliaji kwa kutumia pump ya mafuta na kila siku lazima tununue mafuta na kama hakuna hela ya mafuta basi tunanishindwa kumwagilia sababu hatuna njia mbadala hapa kumwagilia mazao yetu." Amesema Beatrice

Japhet Mwenura pia ni mkulima katika kijiji hicho anasema yeye uotesha mbegu moja kwa moja katika shamba lake na licha ya kutumia mfumo huo kwa moja shambani lakini amekuja kubaini  kuna athari za kukumbana na magonjwa ya mimea na wadudu, pamoja na upungufu wa uzalishaji.

"Nimekuja kubaini kwamba ukipanda mbegu moja kwa moja shambani sio vizuri sababu nimekua nikirudia kupanda mbegu wakati wa parizi sababu mbegu nyingine zinakauka kutokana na kushambuliwa na magonjwa au kukauka na jua.

Ningependa kuwa na miche yenye afya bora, lakini kuto kupanda moja kwa moja mbegu shambani kunanifanya niwe na changamoto za udhibiti wa magonjwa na wadudu, na hivyo kushindwa kupata mavuno bora na hali duni ya maisha tunashindwa kumudu kununua solar ndio maana tunatumia pump za mafuta" Amesema Japhet

Beatrice Nyamhokya na Japhet Mwenura ni miongoni mwa wakulima wadogo wanaoendesha shughuli za kilimo cha umwagiliaji kwa kulima mazao ya mboga mboga na matunda katika mkoa wa Mara ambao ukosefu wa elimu ya matumizi ya nishati jua(Solar) katika kupinguza gharama za uendeshaji pamoja na uoteshaji wa mbegu katika kitalu ili kupata miche yenye afya bado ni kikazo kikubwa katika kujikwamua kiuchumi.

Katika kuangazia changamoto za wakulima hawa nimezungumza na Marcelina Lubuva ambaye ni mtaalamu wa maswala ya kilimo kutoka ushirika wa wajasiliamali  wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Sokoine(SUGECO) Kilichopo mkoani Morogoro akizungumzia changamoto hiyo kwa wakulima anasema kupanda mbegu kwenye kitalu kabla ya kuhamishia shambani kunasaidia kuongeza uhai wa miche na kupunguza hatari ya magonjwa na ni muhimu kwa wakulima kumwagilia mazao yao mapema asubuhi, kabla jua halijapanda juu, ili kudumisha unyevunyevu wa udongo kwa muda mrefu na kupunguza hatari ya magonjwa na wadudu.

    

“ Ili kulima kilimo chenye tija kwanza mkulima anashauriwa kupanda mbegu kwenye kitalu kabla ya kupeleka shambani ili kuufanya mmea kukua kwa ustawi na kuepukana na kuathirika na wadudu wanao kula mimiea

Lakini pia katika kumwagilia inatakiwa mkulima amwagilie mazao yake asubuhi na jioni ili kuulinda mmea usiweze kuathirika na joto” Amesema Marcelina

Kwa upande wake Kastuli Morice Dalei ambaye ni mhandisi wa kilimo kutoka katika kutoka ushirika wa wajasiliamali  wa wahitimu wa Chuo Kikuu cha Sokoine(SUGECO) kilimo cha umwagiliaji katika mashamba ya wakulima kwa kutumia nishati ya umeme jua ni suluhisho la kuwaondolea gharama wakulima hasa wenye kipato cha chini.

Amesema matumizi ya nishati ya jua kwa umwagiliaji wa bustani unaweza kuwa suluhisho la gharama nafuu na endelevu. Mfumo wa umwagiliaji wa solar hutumia nishati ya jua kwa ajili ya kuendesha pampu za umwagiliaji, hivyo kupunguza matumizi ya nishati ya umeme na gharama za mafuta. Faida zake ni pamoja na kupunguza gharama za uendeshaji, kupunguza athari za mazingira, na kuboresha upatikanaji wa maji katika maeneo yenye ukosefu wa umeme.

“Hapa SUGECO mwanzoni tulikua tunatumia umeme wa tanesco kumwagilia mazao na kisha tukanunua pump ya mafuta ambayo kwa siku tulikua tunatumia kuanzia lita ishirini ukipiga hesabu unakuta tunatumia gharama kubwa sana kuendesha shughuli hii lakni tangu tumefunga solar gharama za uendeshaji zimepungua sana, tunatumia solar muda wote na nawasihi wakulima watumie solar ili kupunguza gharama” Amesema Kastuli.

Mbinu ya kuotesha mbegu kwenye kitalu kabla ya kuhamishia shambani inabainika kuwa yenye manufaa zaidi kwa wakulima wadogo wadogo, ikilinganishwa na kupanda moja kwa moja shambani. Kwa ushauri wa wataalamu, wakulima wanaweza kuongeza tija na kuboresha mavuno yao kwa kutumia mbinu bora za umwagiliaji, kufuata muda sahihi wa kumwagilia, na kuzingatia matumizi ya nishati ya jua (solar) ili kuboresha hali ya kilimo na kupunguza gharama.

Licha ya takwimu kuonesha kuwa Tanzania bado inawatumiaji wachache wa wa matumizi ya nishati ya umeme jua Serikali kupitia wizara ya kilimo kwa mwaka 2023/2024 ilitenga shilingi bilioni 970.8 kwa ajili ya kuongeza uzalishaji na tija, kuongeza ajira zenye staha na ushiriki wa vijana na wanawake katika kilimo, kuimarisha usalama wa chakula na lishe, kuimarisha upatikanaji wa masoko, mitaji na mauzo na mazao nje ya nchi na kuimarisha maendeleo ya ushirika.

Comments

#maratotv

RAIS RUTTO AAMBATANA NA ODINGA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Kenya Mh William Rutto na mke wake wamewasili nchini China kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Katika ziara hiyo ameambatana na waziri mkuu mstaafu wa nchi hiyo Raila Odinga ambaye pia anapigiwa kampeni ili aweze kushinda nafasi ya Uenyekiti wa AU.

WIZARA YA MALI ASILI YASISITIZA MATUMIZI YA SHERIA NA KANUNI KATIKA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA UHIFADHI

Na.Joyce Ndunguru, Morogoro. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii anaeshughulikia Maliasili, Kamishna wa Polisi Benedict Wakulyamba asisitiza matumizi ya sheria na kanuni katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za uhifadhi. Kamishna Wakulyamba ameyasema hayo leo Septemba 1, 2024 wakati wa ziara ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo Mkoani Morogoro kwa lengo la kuongea na watumishi ili kuimarisha utendaji kazi pamoja na kukagua maeneo ya kazi. "Kama wahifadhi tunapaswa kufahamu sheria zote zinazosimamia masuala ya uhifadhi zilizopo katika Taasisi zetu pamoja na za Taasisi zingine za uhifadhi zilizopo ndani ya Wizara ya Maliasili na utalii" amesema Kamishna Wakulyamba. "Pamoja na kufahamu sheria na kanuni zilizopo ndani ya Wizara yetu, ni vyema kufahamu na kuzingatia sheria nyingine za Nchi ambazo zinatuzunguka ili ziweze kutusaidia katika utekelezaji wa majukumu yetu mfano sheria inayohusiana na ukusanyaji wa vielelezo kuanzia kw...

Rais Dkt. Samia Awasili China Kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano Kati ya China na Africa FOCAC

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Beijing Capital nchini China kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) tarehe 03 Septemba, 2024.

Wananchi Serengeti Wamtaja Dkt Rhimo Nyansaho Kama Chachu ya Maendeleo Kwao

Na Shomari Binda-GMTV  WANANCHI Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wamemtaja Dkt.Rhimo Nyansaho kama chachu ya maendeleo kupitia taasisi yake ya Nyansaho Foundation. Wakizungumza kwa nyakati tofauti na GMTV wananchi hao wamesema kwa kipindi kirefu mchango wake umeonekana katika kuisaidia jamii. Wamesema ukifika Jimbo la Serengeti kila Kata na Kijiji huwezi kukosa mkono wa Dkt.Nyansaho kuchangia na kusaidia jamii kuanzia elimu,afya,maji na masuala mengine ya jamii. Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Mwita Sagati amesema wapo watu wanaojitokeza kusaidia jamii kipindi cha uchaguzi kwa kulenga kupata uongozi lakini imekuwa tofauti kwa Dkt.Nyansaho. Sagati amesema iwapo atajitokeza kuomba nafasi ya ubunge wapo tayari kumpambania na kumchagua ili aweze kuendelea kutoa mchango wake katika kusaidia jamii. " Tunashukuru sana mchango wa Dkt.Nyansaho kwa kuchangia shughuli za maendeleo hapa Serengeti. " Wengine huwa wanakuja nyakati za uchaguzi lakini huyu mchango wake ni ...

Meli ya Mv. Serengeti yapinduka na kuzama katika Bandari ya Mwanza kusini

 Meli Mv.Serengeti imepinduka na kuzama kwenye bandari ya mwanza kusini.  Meli hiyo imepinduka na kuzama disemba 26 majira ya saa Saba za usiku.  Tukio hilo limetokea meli hiyo ikiwa imefungwa katika gati la bandari ya mwanza kusini.  Kampuni ya meli Tanzania(Tashico) imethibitisha meli ya Mv. Serengeti kupinduka na kuzama upande mmoja wa nyuma.  Kwa Mujibu wa Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma cha Kampuni hiyo inaeleza kuwa Tashico imeshirikiana na Timu mbalimbali za Wataalam kutoka Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC), Mamlaka ya Usimamizi wa bandari (TPA) na wadau wengine katika Juhudi za Uokoaji.  Kwa Mujibu wa Taarifa hiyo,Taarifa rasmi ya chanzo cha Tatizo itatolewa Meli hiyo itakapokuwa imeinuliwa na Uchunguzi wa kubaini Tatizo utakapokuwa umefanyika. Meli ya Mv.Serengeti inadaiwa kusitisha safari zake kwenye ziwa Victoria mwaka 2016  Meli ya Mv.Serengeti imepinduka na kuzama katika...

MAKOMANDOO MIAKA 60 YA JWTZ,HAIJAWAHI KUTOKEA

Makomandoo ya jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania (JWTZ)wamekuwa kivutio cha aina yake kwenye kikele cha maadhimisho ya miaka 60 ya tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo. Katika sherehe hizo ambazo zimefanyika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika uwanja huo wa Uhuru Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 1 Septemba, 2024. Rais ameonesha kujivunia na kulipongeza JWTZ kwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya kuanzishwa kwake huku akitumia nafasi hiyo kuwapongeza Marais waliomtangulia kwa kazi kubwa waliyofanya wakati wa uongozi wao kwa kuliongoza vema jeshi hilo.

Mbunge wa Bukoba Vijijini ameaga Sifa Kedekede Kwa Rais Samia

 Na Angela Sebastian; Bukoba  MBUNGE wa jimbo la Bukoba vijijini Dk. Jasson Rweikiza amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa niaba ya wananchi wa jimbo hilo, kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja mawili ambayo ni lango la kutoka na kuingia ndani ya mkoa wa Kagera. Ametoa shukrani hizo wakati akiongea wananchi mbalimbali waliofika katika viwanja vya Rweikiza pre and Primary school iliyoko eneo la Kyetema Bukoba vijijini, kwa kwa ajili ya kumbukizi ya miaka 100 ya kuzaliwa baba wa mbunge huyo aliyekuwa akiitwa Samsoni Rweikiza.  Rweikiza amebainisha kuwa,Dk. Samia Suluhu Hassan ni Rais mwenye upendo amekubali kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya Bukoba Vijijini na ndiyo maana tunasema atakuwa kiongozi wetu kwa awamu nyingine tena,tunapaswa kila mmoja kumuunga mkono. ametaja madaraja hayo kuwa ni Karebe ambalo limetengewa kiasi cha shilingi bil.9.3 kwa ajili ya ukarabati mkubwa kutokana na daraja ...

Jenerali Jacob Mkunda Atembelea Meli Tiba ya China Aridhishwa na Huduma

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda ametembelea meli tiba ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China Peace Ark ili kuona matibabu yanavyofanyika. Jenerali Mkunda amefurahishwa na namna wataalam wa tiba wa Jeshi la China walivyotoa matibabu kwa kushirikiana na wataalam wa tiba wa JWTZ . Meli tiba ya jeshi la China imekuja hapa nchini na kutia nanga kwenye bandari ya Dar Es Salaam kutoa matibabu mbalimbali kwa wananchi ikiwa ni muendelezo wa maadhimisho ya miaka 60 tangu kuanzishwa kwa JWTZ  na ushirikiano wa miaka 60 baina ya JWTZ na Jeshi la Ukombozi la Watu wa  China. Matibabu hayo yalianza kutolewa tarehe 18 Julai 2024 hadi tarehe 22 Julai 2024. Meli tiba hiyo itaondoka hapa nchini tarehe 23 Julai mwaka huu.

AMIRI JESHI MKUU AKAGUA GWARIDE LA MIAKA 60 YA JWTZ

 Mapema leo asubuhi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride Maalumu la Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Uwanja wa Uhuru leo September 01,2024. Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa jeshi la ulinzi la Wananchi Tanzania si jeshi la Uvamizi bali ni jeshi la ulinzi wa Wananchi Tanzania Amewahakikishia wanajeshi kufanya kazi kifua mbele,kuwa amiri jeshi mkuu yuko pamoja nao wakati wote.

Jenerali ameacha alama ya uzalendo na kujitoa kwa ajili ya Taifa

*📌 Serikali itaenzi na kuthamini mchango wake* *📌 Asema Jenerali Musuguri alijitolea kuhakikisha Tanzania inabaki na amani na usalama* *📌 Asema alikuwa mstari wa mbele kuliokoa Taifa* *📌 Aiasa jamii kuacha alama katika maisha ya kila siku* *📌 Dkt. Biteko aongoza mamia ya watu mazishi ya Jenerali Musuguri Butiama* Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa  aliyewahi kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Mstaafu David Bugozi Musuguri alijitolea  kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa na amani, usalama na mshikamano pamoja na kuifundisha jamii  moyo wa dhati wa kuilinda nchi. Dkt. Biteko amesema hayo leo Novemba 4, 2024 Butiama mkoani Mara wakati akiwasilisha salamu za Serikali kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Jenerali Mstaafu Musuguri. “ Katika  uhai wa kila mmoja wetu ni jambo gani mtu atakumbukwa nalo, baba huyu a...