Polisi Mwanza Yajivunia Kupungua Kwa Matukio ya Ukatili wa Kijinsia

GEORGE MARATO TV
0


 Na Dawati la Habari Polisi Mwanza

Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza limefanikiwa kupunguza matukio ya ukatili wa kijinsia kutoka matukio 1140 mwaka jana hadi 1118 mwaka huu sawa na pungufu ya asilimia 22.

Hayo yamebainishwa leo Disemba 10, 2024 na kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Wilbrod Mutafugwa wakati wa kuadhimisha Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika uwanja wa Polisi Mabatini.

Kupungua kwa matukio hayo kumetokana na jitihada zinazofanywa na Jeshi la Polisi kupitia Mtandao wa Polisi wanawake (TPF NET) Dawati la Jinsia na watoto na Polisi kata wa kutoa elimu na kuchukua hatua za kisheria kwa watuhumiwa wa masuala ya ukatili.

Maadhimisho hayo huadhimishwa kila mwaka nchini ifikapo Novemba 25 hadi Disemba 10 ikiambatana na siku ya haki za binadamu.

Siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia ziliasisiwa na aliyekuwa katibu mkuu wa umoja wa Mataifa awamu ya 7 Kofi Annan mwaka 2006 ya kutaka dunia itambue kuwa lipo tatizo kubwa la ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto.

Hii ilitokana na kuazimishwa na kituo cha umoja wa mataifa wa wanawake kupinga ukatili wa wanawake wanaharakati wa kisiasa waliouawa Mirabal Sisters mwaka 1960 kutokana na amri ya aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Rafael Trujillo katika Jamhuri ya watu wa Dominica.

Naye mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi ameitaka Jamii kupaza sauti kwa pamoja kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Sambamba na hayo wadau mbalimbali waliohudhuria maadhimisho hayo wametaja baadhi ya sababu zinazosababisha uwepo wa ukatili wa kijinsia ikiwemo afya ya akili na kuliomba Jeshi la Polisi kuendelea kukemea na kuchukua hatua za kisheria kwa watuhumiwa wa vitendo hivyo.













Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top